LHRC J.K KWANINI KUIVUNJA TUME YA MABADILIKO YA KATIBA
KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimestushwa na kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kuivunja mapema Tume ya Mabadiliko ya Katiba na kusema haikustahili kuvunjwa wakati Bunge Maalumu la Katiba bado linaendelea.
Kauli hiyo ilitolewa mjini hapa juzi na mjumbe wa Kamati Maalumu ya Katiba kutoka LHRC, Exavery Lwaitama, alipokuwa akitoa mada kwenye warsha ya jukwaa la mchakato wa katiba mpya, ulioandaliwa na Mtandao wa Kufuatilia Sera Mwanza (MPI), na kuwashirikisha viongozi wa asasi na mashirika mbalimbali kutoka wilaya za Ukerewe, Nyamagana, Ilemela, Magu za mkoani Mwanza, pamoja na Wilaya ya Karagwe, Kagera.
Lwaitama ambaye pia ni mhadhiri mwandamizi mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), alisema kuvunjwa kwa tume hiyo wakati Bunge la Katiba halijamalizika, ni kuharibu mwenendo na mchakato mzima wa Watanzania kupata katiba wanayoitaka.
Alisema haiwezekani Rais Kikwete aivunje tume hiyo kisha majukumu yake kuchukuliwa na serikali ambayo tangu awali imekuwa ikikataa kutungwa kwa katiba mpya. “Utavunjaje tume wakati Bunge la Katiba halijaisha? Sasa hii rasimu ya katiba inayojadiliwa bungeni itasimamiwa na nani kama tume imevunjwa? Itawezekanaje isimamiwe na serikali ambayo tangu mwanzo haitaki kutungwa kwa katiba mpya?
“Tunakumbuka mwaka 2011 Mwanasheria Mkuu wa Serikali (Jaji Fredrick Werema), na viongozi wengine wa serikali walikataa kutungwa katiba mpya. Sasa leo rais anaivunja tume, hivi tunategemea kuna upatikanaji wa katiba hapa?” alihoji Lwaitama.
Wakizungumza katika warsha hiyo, viongozi wa mashirika na asasi hizo, walisema hawaoni mwelekeo wa Watanzania kupata katiba mpya wanayoitaka, hivyo wakasema ni bora Bunge hilo likavunjwa, ili kuepusha matumizi mabaya ya fedha.
Mratibu wa MPI, Jonathan Kassim, alisema wameandaa warsha hiyo ili kutoa sauti ya pamoja kwa asasi na mashirika hayo kuhusu mwenendo wa Bunge hilo na kuwaomba wajumbe na serikali kwa ujumla kuwatendea haki wananchi kwa kupitisha maoni yao.
Kauli hiyo ilitolewa mjini hapa juzi na mjumbe wa Kamati Maalumu ya Katiba kutoka LHRC, Exavery Lwaitama, alipokuwa akitoa mada kwenye warsha ya jukwaa la mchakato wa katiba mpya, ulioandaliwa na Mtandao wa Kufuatilia Sera Mwanza (MPI), na kuwashirikisha viongozi wa asasi na mashirika mbalimbali kutoka wilaya za Ukerewe, Nyamagana, Ilemela, Magu za mkoani Mwanza, pamoja na Wilaya ya Karagwe, Kagera.
Lwaitama ambaye pia ni mhadhiri mwandamizi mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), alisema kuvunjwa kwa tume hiyo wakati Bunge la Katiba halijamalizika, ni kuharibu mwenendo na mchakato mzima wa Watanzania kupata katiba wanayoitaka.
Alisema haiwezekani Rais Kikwete aivunje tume hiyo kisha majukumu yake kuchukuliwa na serikali ambayo tangu awali imekuwa ikikataa kutungwa kwa katiba mpya. “Utavunjaje tume wakati Bunge la Katiba halijaisha? Sasa hii rasimu ya katiba inayojadiliwa bungeni itasimamiwa na nani kama tume imevunjwa? Itawezekanaje isimamiwe na serikali ambayo tangu mwanzo haitaki kutungwa kwa katiba mpya?
“Tunakumbuka mwaka 2011 Mwanasheria Mkuu wa Serikali (Jaji Fredrick Werema), na viongozi wengine wa serikali walikataa kutungwa katiba mpya. Sasa leo rais anaivunja tume, hivi tunategemea kuna upatikanaji wa katiba hapa?” alihoji Lwaitama.
Wakizungumza katika warsha hiyo, viongozi wa mashirika na asasi hizo, walisema hawaoni mwelekeo wa Watanzania kupata katiba mpya wanayoitaka, hivyo wakasema ni bora Bunge hilo likavunjwa, ili kuepusha matumizi mabaya ya fedha.
Mratibu wa MPI, Jonathan Kassim, alisema wameandaa warsha hiyo ili kutoa sauti ya pamoja kwa asasi na mashirika hayo kuhusu mwenendo wa Bunge hilo na kuwaomba wajumbe na serikali kwa ujumla kuwatendea haki wananchi kwa kupitisha maoni yao.
Posted in
Jamii
Related posts:
If you enjoyed this article, subscribe to receive more great content just like it.
Popular Posts
-
Na Yericko Nyerere (Mwanahalisi Forum) Usiku wa tarehe 12 Januari 1964 kundi la watu 300 walikitwaa kisiwa cha Unguja wakiongozwa na mtu a...
-
Niliwahi kutoa ahadi kuwa nitaweka sababu nzito Tano ambazo mimi binafsi naziona zinafaa sana kumtathmini Edward Lowasa kama Rais ambaye T...
-
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akionyeshwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Eng. Muss...
-
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA, Mama Salma Kikwete akiwasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma na ku...
-
</a Na Yericko Nyerere Taarifa ya gazeti la majira la mwezi wa 11 (sikumbuki tarehe) iliyosema Zitto katishiwa maisha, ilipelekea jeshi ...
-
THE Monduli Constituency MP, Edward Lowassa (b. Aug. 26,1953), has been causing a political storm of gargantuan proportions across the Tan...
-
Teller Ref No. UTT -MFI/TL/0414/15 Company:UTT Microfinance Plc Location:Dar Es Salaam POSITION DESCRIPTION: The UTT Microfinance Plc now i...
-
A list of famous people, chosen mainly from the Ninenteenth, Twentieth or Twenty First Century. This list includes famous actors, politici...
-
The jet, christened ‘The Great Rift Valley’ is the first of six 787s which Kenya Airways has ordered as part of its mordernisation ...
-
KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimestushwa na kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kuivunja mapema Tume ya Mabadiliko ya Katiba n...
Kuhusu sisi
Powered by Blogger.
Recent Stories
Ukurasa wetu wa Facebook
Wadhamini
Blog Archives
Recent Comments
Tag Cloud
0 comments for this post
Leave a reply