Yanga yawapa kadi nyekundu wanne
KATI ya mechi tisa ambazo Yanga imecheza kwenye mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara, michezo yao minne iliwasababishia baadhi ya wachezaji wa timu pinzani watolewe kwa kadi nyekundu.
Yanga imebakiza mechi nne mkononi dhidi ya Kagera Sugar, JKT Oljoro, JKT Ruvu na Simba.
Timu ambazo ziliwapoteza wachezaji wao kwa kadi nyekundu ni Mtibwa Sugar ambayo mshambuliaji wake, Abdallah Juma, alitolewa kwa kadi nyekundu katika mechi iliyochezwa mjini Morogoro ambapo timu hizo hazikufungana.
Azam FC ilimpoteza beki wa kulia, Erasto Nyoni baada ya kupewa kadi nyekundu katika mechi iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Yanga alifungwa mabao 2-1.
Sekeseke hilo, limewakuta pia Mgambo Shooting Jumapili iliyopita walipoifunga Yanga mabao 2-1, mshambuliaji wao Mohamed Neto alipewa kadi nyekundu.
Mchezaji mwingine ni Steven Mazanda wa Mbeya City, yeye alionyeshwa kadi nyekundu na timu yake ikafungwa bao 1-0 Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Mechi za Yanga ambazo wapinzani wao walitoka salama kwenye mzunguko huu wa pili ni dhidi ya Coastal Union walipocheza Uwanja wa Mkwakwani, Tanga wakashindwa kufungana.
Mechi nyingine waliifunga Ashanti mabao 2-1 jijini Dar es Salaam, walipoishinda Rhino nyumbani kwao Tabora mabao 3-0. Pia katika ushindi wa Yanga wa mabao 5-0 walipoifunga Prisons Mbeya na walipoipiga Ruvu Shooting mabao 7-0 Uwanja wa Taifa.
Kocha mzawa, Kenny Mwaisabula, ametoa ufafanuzi wa kitaalamu wa suala hilo na kusema: “Hii ni kwa sababu Yanga wana wachezaji wenye kasi na inajulikana kuwa inao washambuliaji wazuri.
“Kwa maana hiyo, ili kuidhibiti kasi ya wachezaji kama Msuva (Simon), Ngassa (Mrisho), Okwi (Emmanuel) au Kiiza (Hamis) ni lazima uwachezee faulo ambazo ndiyo zinazalisha kadi nyekundu.
“Kwa kawaida, mabeki huwa hawataki kufungwa na ndiyo maana mambo kama hayo yanatokea.”
Yanga ni ya pili kwenye msimamo wa ligi, ina pointi 46, wakati Azam ndiyo inaongoza kwa pointi 53. Mbeya City ni ya tatu ina pointi 45 wakati Simba ni ya nne inazo 36.
Related posts:
If you enjoyed this article, subscribe to receive more great content just like it.
Popular Posts
-
Na Yericko Nyerere (Mwanahalisi Forum) Usiku wa tarehe 12 Januari 1964 kundi la watu 300 walikitwaa kisiwa cha Unguja wakiongozwa na mtu a...
-
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akionyeshwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Eng. Muss...
-
Niliwahi kutoa ahadi kuwa nitaweka sababu nzito Tano ambazo mimi binafsi naziona zinafaa sana kumtathmini Edward Lowasa kama Rais ambaye T...
-
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA, Mama Salma Kikwete akiwasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma na ku...
-
THE Monduli Constituency MP, Edward Lowassa (b. Aug. 26,1953), has been causing a political storm of gargantuan proportions across the Tan...
-
Teller Ref No. UTT -MFI/TL/0414/15 Company:UTT Microfinance Plc Location:Dar Es Salaam POSITION DESCRIPTION: The UTT Microfinance Plc now i...
-
The jet, christened ‘The Great Rift Valley’ is the first of six 787s which Kenya Airways has ordered as part of its mordernisation ...
-
A list of famous people, chosen mainly from the Ninenteenth, Twentieth or Twenty First Century. This list includes famous actors, politici...
-
KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimestushwa na kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kuivunja mapema Tume ya Mabadiliko ya Katiba n...
Kuhusu sisi
Powered by Blogger.
Recent Stories
Ukurasa wetu wa Facebook
Wadhamini
Blog Archives
Recent Comments
Tag Cloud




0 comments for this post
Leave a reply