Mugabe asusia mkutano kuhusu CAR
Viongozi wa Ulaya na Afrika wanatarajiwa kuanza kujadili mgogoro unaotokota katika Jamuhuri ya Afrika ya Kati, katika mkutano maalum unaofanyika kando na kongamano la viongozi wa Ulaya mjini Brussels.
Rais Robert Mugabe amesusia kongamano hilo baada ya Muungano wa Ulaya kukataa kumwondolea marufuku ya muda ya Visa mkewe Grace.
Bwana Mugabe aliungwa mkono na Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma, ambaye pia ameamua kuususia mkutano huo kama ishara ya kumuunga mkono Mugabe.
Zuma alisema kuwa muda umewadia wa Ulaya kukoma kuwaangalia waafrika kama sio watu.
Muungano wa Ulaya tayari umezindua kikosi cha jeshi lake nchini CAR, na kuelezea mipango yake kutuma wanajeshi 1,000 kuwasaidia wanajeshi wa Afrika na wale wa Ufaransa wanaoshika doria nchini humo.
Umoja wa Mataifa umeonya kuwa waisilamu 19,000 wanakabiliwa na tisho la kuuawa nchini humo.
Maswala ya Uchumi na Uhamiaji pia yatapewa kipaombele kwenye mkutano huo.
Viongozi 30 wanatarajiwa kuhudhuria kongamano lenyewe wakiwemo marais wa Afrika.
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon atahudhuria mkutano kuhusu CAR pamoja na viongozi wa Afrika na wale wa Muungano wa Ulaya.
Ameahidi kufAnya kila awezalo kuhakikisha anaimarisha juhudi za kukabiliana na migogoro ya kimataifa.
Related posts:
If you enjoyed this article, subscribe to receive more great content just like it.
-
Na Yericko Nyerere (Mwanahalisi Forum) Usiku wa tarehe 12 Januari 1964 kundi la watu 300 walikitwaa kisiwa cha Unguja wakiongozwa na mtu a...
-
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akionyeshwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Eng. Muss...
-
Niliwahi kutoa ahadi kuwa nitaweka sababu nzito Tano ambazo mimi binafsi naziona zinafaa sana kumtathmini Edward Lowasa kama Rais ambaye T...
-
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA, Mama Salma Kikwete akiwasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma na ku...
-
THE Monduli Constituency MP, Edward Lowassa (b. Aug. 26,1953), has been causing a political storm of gargantuan proportions across the Tan...
-
Teller Ref No. UTT -MFI/TL/0414/15 Company:UTT Microfinance Plc Location:Dar Es Salaam POSITION DESCRIPTION: The UTT Microfinance Plc now i...
-
The jet, christened ‘The Great Rift Valley’ is the first of six 787s which Kenya Airways has ordered as part of its mordernisation ...
-
A list of famous people, chosen mainly from the Ninenteenth, Twentieth or Twenty First Century. This list includes famous actors, politici...
-
KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kimestushwa na kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kuivunja mapema Tume ya Mabadiliko ya Katiba n...



0 comments for this post
Leave a reply