"Habari zilizopewa uzito"
Habari Mbali mbali

MJADALA WA RASIMU YA KATIBA SURA YA KWANZA NA SITA

Wadau, amani iwe kwenu. .., Kwa mujibu wa Ratiba ya vikao vya Bunge Maalum ambapo nimepata nakala yake, ni kwamba kuanzia juzi tarehe 31 Machi 2014, Bunge Maalum limeanza vikao vya kujadili vifungu vya Rasimu ya Katiba kupitia kwenye mijadala ya Kamati za Bunge Maalum. Mijadala hiyo itahitimishwa Jumamosi tarehe 12 Aprili 2014 ambapo Bunge Maalum litapiga kura kufanya maamuzi juu ya vifungu hivyo. Mijadala hiyo kwa mujibu wa vifungu hivyo inahusu Sura ya Kwanza na ya Sita. Zimechaguliwa sura mbili ili kukidhi matakwa ya kikanuni. Aidha, Wamechagua sura ya Sita badala ya Sura ya Kwanza na ya Pili si kwa vile Mwenyekiti anaitwa Sammuel Sita na hivyo kupendekeza sura ya sita ianze kwa lengo la kulipa heshima jina lake, la hasha. Sura hizo mbili zimeteuliwa na Kamati ya Uongozi kutokana na umuhimu wake. Kwani sura hizo mbili zinahusu hatima ya nchi yetu. Pia sura hizo ndizo sura mama za Rasimu ya Katiba hivyo ni vema zikajadiliwa kwanza ili maamuzi yatakayofikiwa juu ya sura hizo ndiyo yatakayotoa muelekeo wa mjadala mzima wa Rasimu ya Katiba. Mjadala mkubwa utakaoibuka kwenye Kamati na kwenye vikao vya Bunge Maalum unatarajiwa kuwa ni juu ya muundo wa muungano. Hapa tunatarajia kuwa na mjadala mkali na wakati mwingine wabunge watapandwa na jazba hali itakayowapelekea kukiuka baadhi ya kanuni za Bunge Maalum. Watafanya hivyo kwa lengo la kutetea misimamo yao kuhusu muundo wa muungano. Kwa hali ilivyo hivi sasa, mchuano mkali ni baina ya wale wanaotaka muundo wa Serikali Mbili kama ilivyo kwenye Katiba iliyopo na wale wanaotaka muundo wa Serikali Tatu kama ulivyoainishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Naamini kuwa hata humu ndani ya mitandao ya kijamii pia watu tumegawanyika kwa muktadha huo. Pia naamini kuwa kuna waumini wa serikali Moja na Serikali Nne. Yote hayo ni mawazo ya wabunge na wananchi. Hata hivyo mwisho wa siku ni kwamba ni muundo mmoja tu ndio utakaopitishwa tarehe 12 Aprili 2014 kwa kura ya wazi na siri kutegemeana na utashi wa mbunge. kwa lengo la kupanuana mawazo juu ya mjadala huu, nawaalika wachambuzi mbalimbali ambao wataweka hoja za msingi hasa juu ya muundo wa muungano. Watu tujadili kwa hoja na si kuendekeza ushabiki wa kisiasa. Wachangiaji ni vema tukajikita kwenye hoja. kejeli na dharau dhidi ya aina fulani ya muungano na wafuasi wake hazitasaidia kwenye mjadala huu. Pia wachambuzi ambao watasimama kati kwa kati watatusaidia sana kupata mawazo ya pande zote mbili kwa ufasaha. Wale watakaoamua kuweka bayana misimamo yao wanapaswa pia kueleza kwa nini wanaona kuwa muundo wanaoupendekeza ni bora zaidi. Naomba Kuwasilisha.....

Share and Enjoy:

0 comments for this post

Leave a reply

Pata Habari papo kwa hapo
Weka anuani pepe yako hapa ili upate habari punde tunapo ziweka katika EAfrican Blog!
Subscribe via RSS Feed subscribe to feeds
wadhamini
Designed by Cebanet.netDesigned by Cebanet.netDesigned by Cebanet.net
Designed by Cebanet.netDesigned by Cebanet.netDesigned by Cebanet.net
Popular Posts
Recent Stories
Ukurasa wetu wa Facebook
Wadhamini
Search
Archives
Blog Archives
Recent Comments
Tag Cloud